MAREHEMU CHRIS MWAMBONDA KUZIKWA LEO SAA 8 MCHANA HUKO GOBA
Mwandishi
Mwandamizi wa Habari za Michezo, Chris Mwambonda aliyefariki usiku wa
kuamkia jana jijini Dar es Salaam, anatarajiwa kuzikwa leo Jumatatu
saa 8 mchana nyumbani kwa mama yake mzazi huko Goba. Kwa mawasiliano ya
kuweza kufika na kushiriki mazishi hayo, maelekezo yatatolewa kwa yeyote
atakayehitaji kufanya hayo kupitia namba ya simu: 0758 333 436.
Pichani, Mwambonda kushoto katika moja ya matukio aliyoshiriki enzi za
uhai wake ambapo hapa anaonekana akikabidhiwa na Mkurugenzi wa Baraza la
Michezo Tanzania (BMT), Leonard Thadeo, cheti cha ushiriki wa mafunzo
yaliyowashirikisha Wahariri wa Michezo yaliyofanyika Juni 10 2010.

No comments:
Post a Comment