KOCHA CAMEROON ATAKA ETO'O AVULIWE BEJI YA UNAHODHA
Mshambuliaji na nahodha wa Cameroon, Samuel Eto'o
YAOUNDE, Cameroon
KOCHA
wa timu ya taifa ya Cameroon, Denis Lavagne ametaka mshambuliaji Samuel
Eto'o anyang’anywe unahodha wa kikosi hicho pindi atakaporejea kikosini
kutoka kufungiwa na Shirikisho la Soka la nchi hiyo (CFF).
Eto'o
alifungiwa kutocheza timu ya taifa kwa miezi minane kwa kuongoza mgomo
Novemba mwaka jana, wakati Cameroonilipokataa kucheza kirafiki na
Algeria kwa sababu ya kushinikiza utekelezaji wa malipo ya posho
walizoahidiwa.
Katika
barua yake kwa CFF, Lavagne raia wa Ufaransa amelitaka shirikisho hilo
kufanya maamuzi juu ya beji ya unahodha wa Eto’o kabla ya mechi za
mwisho za hatua ya awali kufuzu Mataifa Afrika 2013 dhidi ya Cape Verde
Islands hapo Septemba na Oktoba.
"Kwa hiyo,
tunaomba mkutano wa kuthibitisha uteuzi wa nahodha mpya wa timu ya taifa
na msaidizi," aliandika Lavagne katika barua aliyoionesha kwa vyombo
vya habari vya Cameroon.
Aidha,
Lavagne alilalamika kwamba mshahara wake wa dola 245,000 hajalipwa hadi
sasa na CFF, na kwamba makubaliano katika mkataba yalitaka alipwe pesa
hiyo kwa pamoja.
Lavagne,
aanakumbukwa kwa tamko lake la hivi karibuni alilitoa la kulionya
shirikisho la soka la nchi hiyo kwa kukosa heshima kwa waziri wa
serikali anayehusika na michezo.
Mfaransa
huyo alipewa mikoba ya kuinoa Cameroon mwaka jana, baada ya vigogo hivyo
vya soka kumtimua Mhispania Javier Clemente aliyeshindwa kuipeleka nchi
hiyo katika fainali zilizopita za Mataifa Afrika 2012 huko Equatorial
Guinnea na Gabon.

No comments:
Post a Comment