Friday, June 21, 2013


EXCLUSIVE Interview na MISS YUNAR MAGICION.

Miss Yunar Magicion ni msanii wa Kitanzania anayekuja kwa kasi katika tasnia ya Muziki hapa nchini, kwa track zake mbili alizozitoa “Nisamehe aliyomshirikisha Ben Pol” na “Hoi aliyomshirikisha Drea” ni ushahidi tosha kuwa Miss Yunar ni moto wa kuotea mbali, Baada ya kuliona hilo nilifanya jitihada za kumtafuta Miss Yunar Magicion ili kufanya naye Interview, na hivi ndivyo ilivyokuwa:

Anaclet: Mambo vipi Miss Yunar, uko poa?

Miss Yunar: Poa tu mkaka, mzima wewe?

Anaclet: Mi nipo njema sana, Miss Yunar unaweza kutupa japo kwa ufupi historia yako?
Miss Yunar: About Music or what?

Anaclet: Yes, about music.

Miss Yunar: Eeh.. tangu mwaka 2011 mwezi wa 10 nilipomaliza Elimu yangu ya Sekondari ndipo nilipoamua kujihusisha na Muziki, na safari yangu ya kwanza katika muziki ilianzia katika kituo kimoja kinachofahamika kama “mkubwa na wanawe” ambapo nilikaa mpaka mwaka jana mwezi wa 8 na ndipo nikahama na kwenda kwa “Sheddy Clever – BURN RECORD” nikafanikiwa kutengeneza nyimbo yangu iitwayo “NISAMEHE”, kwa Sheddy pia nilikaa kwa muda mfupi, na mpaka sasa nipo mwenyewe sina management, na nimefanikiwa kurekodi nyimbo zingine mbili katika studio nyingine iitwayo “NATAL RECORD” iliyoko Mburahati jijini Dar es Salaam chini ya Producer ABBAH PROCESS..

Anaclet: Idea ya kutunga wimbo wa Nisamehe uliomshirikisha Ben Pol uliupata wapi?

Miss Yunar: Ni idea yangu mwenyewe.

Anaclet: Kwanini uliamua kumshirikisha Ben Pol katika huo wimbo wako wa kwanza?

Miss Yunar: Ni ushauri na maamuzi ya producer, alivyomaliza kuitengeneza huo wimbo akaona ni bora ashirikishwe msanii wa kiume ambaye ni Ben Pol.

Anaclet: Miss Yunar, wewe ni msanii unayekuja kwa kasi sana katika tasnia hii ya muziki nchini Tanzania, je ni vikwazo gani umekuwa ukikumbana navyo?

Miss Yunar: Vikwazo ni vingi sana ten asana, inafikia kipindi natamani  hata nikate tama lakini nasema hapana coz sanaa ni kazi yangu na ndiyo Mungu aliyonipangia so siwezi kuiacha mfano meneja au mtu yoyote ambaye ana ufahamu vizuri njia za muziki, ukimpelekea kazi yako kwa lengo la kutaka kusaidiwa lazima atatanguliza suala la mapenzi mbele, nadhani hilo halina ubishi na sidhani kama kuna msanii wa kike asiyefanyiwa hivyo na vinginevyo.

Anaclet: Na wewe kama msanii mwenye malengo makubwa mbeleni, unakabiliana vipi na vikwazo kama hivyo?

Miss Yunar: Daah.. me najua nini nafanya na nini nahitaji katika maisha yangu ya muziki, kwahiyo siwezi kukubali kufanya kitu kibaya kwasababu ya msaada wake.

Anaclet: Na kwanini uliamua kujiita Miss Yunar?

Miss Yunar: Kwanza kabla ya kujiita “miss Yunar”, mimi nilikuwa najiita “Yunar” ila baada ya kufanya wimbo na Ben Pol, ukiusikiliza vizuri mwishoni Ben Pol anamalizia kwa kutaja “Miss Yunar” ndipo kila mtu alipokuwa akiusikiliza ule wimbo lazima aniite jina la Miss Yunar na hapo ndipo hilo jina lilipoanzia.

Anaclet: Baada ya kutoa track zako mbili, jamii inayokuzunguka inakuchukuliaje? Coz kuna wasanii wakishatoka wanaanza kuonyesha dharau na majivuno, hii wewe kwako lipoje?

Miss Yunar: Kwa upande wangu mimi sipo hivyo kabisa coz sioni faida ya mimi kuwa hivyo, yaani jamii yangu naishi nayo vizuri na bila matatizo yoyote…sina dharau wala majivuno.!

Anaclet: Hongera sana Miss Yunar,  kuna wasii wengi sana hapa nchini na wenye majina makubwa, unaweza kuniambia ni wasanii gani unawakubali zaidi?

Miss Yunar: Kwa upande wa wasanii wa kike ni LADY JAYDEE, PIPI na LINAH na kwa wasanii wa kiume ni BEN POL, Q CHILLAH, PROFESOR J na MABESTE.

Anaclet: Nini malengo yako kimuziki baada ya miaka mitatu au mitano ijayo? Au sisi mashabiki wako tutegemee nini kutoka kwako ?

Miss Yunar : Kwanza kabisa bado nahitaji support kutoka kwa mashabiki, mashabiki wanisupport mimi katika muziki wangu ili kufanya muziki wangu kusonga mbele na kufikia mpaka level za kimataifa, lakini pia lengo langu kubwa ni Taifa limjue, limfahamu Miss Yunar ni nani na anafanya nini katika tasnia hii ya muziki na baada ya hapo nchi nyingine zinifahamu pia lakini kwanza nyumbani Tanzania, hayo ndo malengo yangu, lakini pia ukiacha hilo nina lengo la kuitangaza nchi yangu kupitia kipaji changu cha muziki..

Anaclet : Unazungumziaje kuhusu gharama za kurecord nyimbo hapa nchini, je haiwabani sana wasanii chipukizi kuweza kurecord nyimbo zao ?

Miss Yunar : Mmh.. kwa upande wangu mimi sijajua kuhusu hilo na sina jibu kamili kwasababu unapozungumzia gharama ya kurecord inategemea na makubaliano kati ya msanii na producer, wakati mwingine mtu anaweza akafanya nyimbo hata free na inategemea labda producer alimkubali sana msanii katika uimbaji na ndipo akaamua kumsaidia lakini kubwa ni makubaliano yao tu.

Anaclet : Kwa kumalizia Miss Yunar, unaiambia nini serikali kuhusu kuwasaidia wasanii wanaochipukia ? na unawaambia nini wapenzi na mashabiki wako ?

Miss Yunar : Daah.. mi kwa kweli naiomba serikali itunyooshee mkono wasanii, iwe karibu na wasanii na iwasaidie kwa hali na mali bila kujali, na pia itambue thamani ya msanii katika nchi na lingine wasanii wenyewe tuonyeshe umoja bila kujali huyu ni star au underground au huyu ni Bongo fleva au Hip Hop, kwa misingi hiyo tutafika mbali, lakin kubwa na la zaidi ni support ya mashabiki ndiyo kil akitu kwangu… kwani bila wao hakuna Yunar.

Anaclet : Thanks Yunar for your time na kukubali kufanya interview na mimi na hii isiwe ndiyo mwisho wa kukubali wito wangu pindi nitakapokuhitaji tena.. mimi na watanzania tupo pamoja na wewe na tutakupa support ya kutosha ili kufikia malengo yako kimuziki and for sure mimi nimekukubali sana.

Miss Yunar : Asante sana, na mimi pia nimekukubali na Mungu akubariki na akusimamie katika kazi yako uifanyayo… !! Amen.

Naam, huyo ndiye Miss Yunar ambaye leo nimefanya naye Interview ili kuweza kujua yeye ni nani na anafanya nini.. Tumpe support basi ili aweze kufika pale ambapo anahitaji kufika katika tasnia hii ya muziki hapa nchini na kimataifa pia. Miss Yunar ameongea mengi sana ila kikubwa anasema  kuwa bila wewe hakuna Yunar.

Usikilize kwa umakini wimbo huu NISAMEHE by Miss Yunar ft Ben Pol na utagundua kipaji halisi cha mwanadada Miss Yunar Magicion.

No comments:

Post a Comment