Tuesday, June 25, 2013

AZAM FC YAANZA MAZOEZI TAYARI KWA MSIMU UJAO WA LIGI KUU BARA




Baada ya mapumziko ya wiki tano kikosi cha Azam FC kimeanza mazoezi rasmi leo kujiandaa na ligi kuu ya vodacom 2013, katika mazoezi yao  Azam FC iliwakosa wachezaji 16 kutokana na sababu mbalimbani, waliokosekana ni wachezaji nane wa timu ya taifa Taifa Stars, wachezaji wanne wa kigeni ambao wameomba ruhusa ya kujiunga na wenzao wiki ijayo.
  David Mwantika aliye na matatizo ya kifamilia kama ilivyo kwa Omary Mtaki anayeuguza baba yake na Himid Mao aliyefiwa na baba yake mkubwa.
 

Waliohudhuria mazoezi ya kwanza leo ni Malika Ndeule, Brian Umony, Jabir Aziz stima, Waziri Salum, Gaudence Mwaikimba, Luckson Jonathan kakolaki, Samih Haji Nuhu, Seif Abdallah Karihe, Wandwi Jackson na Ibrahim Mwaipopo
 

Mchezaji pekee ambaye hakufika mazoezini na hakuna taarifa zozote juu ya kukosekana kwake ni Said Morad Mweda.






No comments:

Post a Comment