Thursday, June 20, 2013

MAADHIMISHO YA SIKU YA UTUMISHI WA UMMA BARANI AFRIKA 2013 YAENDELEA MJINI ACCRA

Mkuu wa Kitengo cha Mikopo wa Wizara ya Fedha kutoka kwa Mhasibu Mkuu wa Serikali Bi. Christine Ngonyani akiwa na watumishi wa wizara ya fedha akifafanua kuhusu mikopo inayotolewa na wizara ya fedha.
Afisa Maendeleo ya Jamii Mwandamizi Bw. William Ghump akifafanua jambo kuhusu Mkakati wa kukuza uchumi na kuondoa umasikini kwa wananchi waliotembelea Banda la Wizara ya Fedha.
Mkuu wa Kitengo cha Mikopo wa Wizara ya Fedha kutoka kwa Mhasibu Ghana.Mkuu wa Serikali Bi. Christine Ngonyani akifafanua jambo kwa wananchi wa kijiji hicho.
Msemaji wa Wizara ya Fedha Bi. Ingiahedi Mduma akijibu swali kutoka kwa Mwanajeshi wa Ghana aliyekuwa anataka kujua ni jinsi gani Wizara ya fedha inawasaidia wanajeshi ambao wanataka kujikwamua kiuchumi.Wakushoto kwake ni Bw. Midladjy Maez(Mkatamiti) ambaye ni Maneja wa Mahusiano TRL akisikiliza kwa makini maelezo hayo.
Mkuu wa Kitengo cha Mikopo Bi Christine Ngonyani akiwa na Miriam Mnzava kutoka kwa Mhasibu Mkuu wa Serikali pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Bi. Ingiahedi Mduma wakiwapatia huduma wakuu wa jeshi la Magereza la nchini Ghana.
Mkuu wa Kitengo cha Mikopo Wizara ya Fedha kutoka kwa Mhasibu Mkuu wa Serikali Bi. Christine Ngonyani akiwa na watumishi wa wizara ya fedha walipotembelewa na Bw. Pascal Mugabe ambaye ni Afisa Tawala Rasilimali Watu wa Idara ya Utawala, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambaye yupo Nchini Ghana kwa masomo ya elimu ya juu(Phd) .
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Mhe. Celina O. Kombani alipotembelea banda la Wizara ya fedha na kuelezea jinsi alivyofurahishwa na ushiriki wa Wizara ya fedha katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Mhe. Celina O. Kombani akisani kitabu cha wageni. Picha zote na Scola Malinga – Hazina- Tanzania.

No comments:

Post a Comment