Wednesday, June 26, 2013

JUMA KASEJA ATUPIWA VILAGO RASMI SIMBA, ATOWEKA MAZOEZINI, ALAANI KUFANYIWA FUJO MORO

KLABU ya Simba ya Jijini Dar es Salaam, leo imetangaza rasmi kumtema Nahodha wake ambaye pia ni Nahodha wa timu ya Taifa na Simba, Juma Kaseja,  ambaye alikuwa akiwaumiza vichwa viongozi wa Klabu hiyo.

Awali Kaseja, alikuwa akikaririwa na Vyombo vya habari kuwa hajajua 
hatima yake na Klabu ya Simba na kuhusishwa ukimya wake na kuhamia Timu ya Azam, ambao awali walionyesha nia ya kumhitaji.

Lakini alipohojiwa Kaseja, alisema kuwa bado alikuwa akihitaji 
kupumzika ili kujua kuwa atasaini tena sima ama la, na kwa upande wa 
Azam, walipohojiwa kuhusiana na hilo, nao waliruka Kimanga kuonyesha 
nia ya kumhitaji Kipa huyo namba moja wa Simba.
Hili la kutunguliwa mabao kama haya si sababu za kutemwa, kipa 
huyu nambamoja, lazima kuna sababu iliyojificha nyuma ya pazia, 
'Kisiasa zaidi', na wala haiingii akilini kuwambiwa Kaseja ameshuka 
kiwangi kama wanavyoeleza mashabiki na viongozi wa Simba.

Akizungumza na mtandao huu Ofisa Habari wa Simba, Ezekiel 
Kamwaga alisema kuwa mpaka wanawasili kwenye Uwanja wa Kinesi 
jioni ya leo kwa ajili ya mazoezi ya timu hiyo, Kipa huyo hakuwepo 
mazoezini ambapo Ezekile, alisema kuwa inawezekana ameathirika kisaikolojia baada ya kufanyiwa vurugu na mashabiki wa Simbo mkoani Morogoro wiki iliyopita.
Nao Uongozi wa Klabu hiyo, leo umeweka wazi kuwa hawatakuwa na
 Kipa huyo katika msimu ujao, na kutangaza rasmi kuwa wamevunja 
ndoa yao rasmi leo, bila kueleza sababu za kumuacha kipa huyo, huku ikielezwa kuwa huenda ikawa ni dau alilohitaji kipa huyo, jambo ambalo limekanushwa na Uongozi huo.

Hatimaye uongozi wa klabu ya Simba kupitia kwa mwenyekiti wa 
kamati ya usajili Zacharia Hans Pope umetangaza rasmi kuachana 
na mlinda mlango mkongwe wa timu hiyo  Juma Kaseja.
Hans Pope ameyasema hayo katika  kipindi cha michezo  cha Radio 
One jijini Dar es Salaam.
Kaseja akifungwa bao katika moja ya mchezo wake.
Amesema hawatomuongezea mkataba Kaseja na wamempa baraka za 
kutafuta timu nyingine.

 Kwa muda mrefu Simba ilikuwa ikisuasua kumpa mkataba Kaseja 
aliyeidakia Simba kwa takribani miaka 10, na hatimaye leo 
wamethibitisha rasmi kumuacha Kaseja.

“Juma ndio basi tena kaka, Kasema yeye na Simba basi, 
amesononeshwa mno na jinsi alivyodhalilishwa baada ya mechi ya Morogoro,”alisikika akisema mchezaji mmoja wa Simba baada ya 
mazoezi Kinesi leo.

Kaseja alitukanwa na kutishiwa maisha na mashabiki wa Simba 
baada ya mechi dhidi ya Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Jamhuri, 
Morogoro wakimtuhumu kufungwa mabao ya kizembe.
Milovan, akiwa hoi katika moja ya mchezo akiwa Mocha wa simba.
Ikumbukwe ni hivi karibuni tu Klabu hiyo, ilimtupia vilango aliyekuwa 
Kocha Mkuu wake, Milovan Circkovic, kwa madai ya kutotimiza malengo
 ya Klabu hiyo kwa kufanya vizuri katika michezo ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara iliyomalizika hivi karibuni, na sasa leo ni zamu ya Juma Kaseja, huku ikiwa tayari imeshafanya hivyo kwa kuwatoa kwa mkopo wachezaji wake, Vipenzi vya mashabiki wa timu hiyo, Haruna Moshi 'Boban' aliyepelekwa katika timu ya Coastal Union ya Tanga, na Juma Nyoso, huku ikitabiriwa anayeguata akawa ni Amir Maftah, ambaye ametetewa na Ofisa habari wa timu hiyo kuwa hayupoa mazoezini kwa sabau ana ruhusa maalum kutokana na kufunga ndoa hivi majuzi.
Juma Kaseja katika moja ya kazi nzuri aliyoifanya akiwa na Simba msimu wa 2012.

No comments:

Post a Comment