Friday, June 29, 2012

 Kocha wa ngumi wa Kambi ya mazoezi ya Big Right, Ibrahim (katikati) akiwa na mabondia wake wakati akiwasimamia katika Kambi yao ya mazozi ya pamoja kama timu kujiandaa na mapambano yao yanayotarajia kufanyika Julai 15 katika Ukumbi wa DDC Kariakoo, jijini Dar es Salaam, mwaka huu.
********************************************

KATIBU wa Vijana wa CCM Kata ya Kinondoni, Rehema Mbegu, ameahidi kutoa zawadi ya Baiskeli kwa Mabondo wa Klabu ya Mazoezi ya Big Right ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam, iwapo watashinda katika mapambano yao yanayotarajia kufanyika hivi karibuni, ili kuwa moyo zaidi vijana kuupenda mchezo wa Masumbwi.

Rehema mbegu, mara kadhaa amekuwa akishirikiana na vijana wa Kata yake katika masuala mbalimbali ya Kijamii na ya kuendeleza michezo, ambapo amekuwa karibu zaidi na vijana wa rika zote na kuwapa sapoti kubwa ikiwa ni pamoja na kuwapa ushauri kujishughulisha na michezo zaidi ili kuepuka kutojiingiza katika mkumbo wa matumizi ya madawa ya kulevya.

Mabondia hao baada ya kuhakikishiwa zawadi nono ya kila atakayeshinda kuibuka na Baiskeli, wamezidi kuwa na morali zaidi na kutoa ahadi zao kwa Katibu huyo kuwa watafia ulingoni hadi kieleweke kwa kutupa mawe ya ukweli kwa wapinzani wao watakaokutana nao siku hiyo ya pambano.

Vijana hi wamekwishaanza kambi yao ya pamoja na kufanya mazoezi ya pamoja kama timu chini ya Kocha wao, Ibrahim Bigright na kuongeza muda wa mazoezi ambapo kwa sasa wanafanya mara tatu hadi kwa siku.

Mabondia hao ambao wanategemea kupanda ulingoni july 15 DDC-kariakoo ni Issa Omar(bigright boxing) atakaechapana na Ramadhan Kumbele, kutoka Kambi ya Matumla, katika uzani wa fly weight, Mwaite Juma kutoka Bigright Boxing,ambaye atapigana mkongwe Anthony Mathias,  katika uzani wa Bantam.

Ambao watakuwa wakisindikiza pambano la ubingwa wa taifa ni kati ya JUMA
FUNDI wa keko na BAINA MAZOLA wa mabibo kutoka kambi ya mzazi


No comments:

Post a Comment