Friday, June 29, 2012


.
Kama ulidhani maafa kama haya ya maafuriko yanaweza kuchukua maisha ya watu kwenye nchi masikini peke yake utakua umekosea, hata Uingereza kwa Malkia hichi kitu kimetokea leo sema tu kuna utofauti mkubwa wa mazingira ya matukio.. wenzetu mvua imenyesha kubwa lakini miundombinu yao inaruhusu kuyasafirisha maji kwa hiyo hata kama yakisimama sio mengi sana.
Gazeti la The sun limethibitisha kwamba mwanaume mmoja anaekadiriwa kuwa na umri wa miaka 90 ambae bado hajatambulika alizombwa na maji ya mvua kubwa iliyonyesha saa nne asubuhi june 28 2012 ambapo mashahidi wamesema mwili wake ulipatikana baada ya msako uliowahusisha police, zima moto na waokoaji wengine ambapo alikutwa kwenye gari lake akiwa amefunikwa na maji.
.
.
.
Mafuriko ya Dar es salaam mwishoni mwa 2011.

No comments:

Post a Comment