Tuesday, June 26, 2012

 Mjini Dortmund, Ujerumani jumamosi 30 Juni 2012 Kikosi kazi cha Ngoma Africa Band aka FFU yenye makao yake kule Ujerumani,wanategemewa kukwea jukwaa la Afro-Ruhr Festival, siku ya jumamosi 30 Juni 2012 mjini Dortmund,Ujerumani.

Bendi hiyo maarufu ya muziki wa dansi barani ulaya inayoongozwa na mwanamuziki Ebrahim Makunja aka kamanda Ras Makunja wa FFU,itapeleka mzimu wake wote wa dansi katika onyesho hilo kubwa la aina yake,washabiki wa muziki katika onyesho hilo wanakumbana "Jino kwa Jino" na makombora ya muziki wa Ngoma Africa band  aka FFU, bendi hiyo kwa sasa inatamba nyimbo zake za "Supu ya Mawe"

,"Uhuru wa Habari" na "Bongo Tambarare" ambazo ipo katika CD ya "BONGO TAMBARARE" pia zinasikika katika kambi yao FFUat www.ngoma-africa.com au http://www.ngoma-africa.com
 
MPIGA SOLO  CHRIS-B WA NGOMA AFRICA BAND

No comments:

Post a Comment