Friday, June 29, 2012

KARIBU KWENYE MAONESHO YA 36 YA BIASHARA YA KIMATAIFA YA DARE SALAAM KWA UDHAMINI WA VODACOM TANZANIA


Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania mwaka huu ni wadhamini Wakuu  ambao wataratibu habari na Mawasiliano katika Maonesho ya 36 ya Biashara ya Kimataifa  ya Dar es Salaam, hivyo wananchi wote wanatangaziwa kufika katika Viwanja vya maonesho hayo,kujione na kupata huduma bora  katika viwanja hivyo.

Meneja Mahusiano wa Vodacom Tanzania Matina Nkurlu(kulia) akimuonesha  Afisa Udhamini na Matukio wa Kampuni hiyo  Ibrahim Kaude,simu ya mkononi  aina ya ZTE s502 yenye Radio na Michezo inayouzwa kwa Tsh 13,000 ikiwa na muda wa maongezi ya Tsh 6,000 ukitaka kupata simu hizo fika katika mabanda ya Vodacom yaliyopo katika viwanja vya maonesho ya 36 ya Biashara Kimataifa(Sabasaba)

Wafanyakazi wa Vodacom Tanzania wakiandaa mabanda katika viwanja vya maonesho ya 36 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam,ambapo wateja watajipatia huduma mbalimbali pamoja na simu ya mkononi  aina ya ZTE s502 yenye Radio na Michezo inayouzwa kwa Tsh 13,000 ikiwa pamoja na  muda wa maongezi ya Tsh 6,000.

No comments:

Post a Comment