Saturday, July 28, 2012

LEO NI LEO KOMBE LA KAGAME FAINALI YANGA NA AZAM NANI KUNYANYUA NDOO


TIMU ya Yanga leo inakabiliwa na kibarua kigumu cha kutetea ubingwa wake wa Kombe la Kagame mbele ya Azam katika mechi ya fainali itakayochezwa uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
 
                                                         Kikosi cha Azam leo

Wakati Yanga chini ya Kocha wake Tom Seintfiet ikitaka kushinda kuweka rekodi ya kulitwaa mara ya tano tangu kuanzishwa rasmi michuano hiyo 1974, Azam wanataka kubeba mara ya kwanza.
Mbali ya Yanga kutaka kutwaa taji hilo mara ya tano baada ya kufanya hivyo mwaka 1975, 1993, 1999 na 2011, Kocha Saintfiet, pia atakuwa akitaka kuanza vizuri kibarua chake.
Aidha, kama Yanga itafungwa itakuwa imetema taji la michuano hiyo ililolitwaa Julai 10, 2011 chini ya Kocha Mganda, Sam Timbe.
 
                                             Kikosi cha Yanga leo
 
Pia, kufungwa kwake itakuwa pigo kubwa kwa uongozi mpya wa klabu hiyo ulioingia madarakani Julai 15 kupitia uchaguzi mdogo chini ya Mwenyekiti wake Yusuf Manji.
Mazingira hayo, yanaifanya Yanga kucheza kufa na kupona kuhakikisha wanashinda sio tu kutetea taji, pia kuanza vizuri kwa kocha na uongozi mpya.

No comments:

Post a Comment