Wednesday, August 15, 2012

.
Ishu ya utoroshaji wa wanyama pori ambayo juzi imefanya watumishi watatu wa maliasili kupigwa chini iliingia kwenye page nyingine bungeni Aug 14 2012 baada ya msemaji rasmi maliasili na utalii mchungaji Peter Msigwa kuhoji uhalali wa kutokamatwa kwa ndege iliyobeba wanyama hao.

Amesema pamoja na kwamba Waziri wa maliasili na utalii ametangaza kuwafukuza kazi maafisa watatu, bado sio suluhisho la kudhibiti ujangili kwani mtandao ulioipitisha ndege ya jeshi la Qatar ni mkubwa na unahusisha wafanyakazi wa uhamiaji, Polisi na baadhi ya vigogo serikalini.

“serikali inahusika kwa sababu kuna wakubwa juu yake na kuwatoa wale ni kafara, watupe taarifa ilikuja hapa kufanya nini na ilipotoka hapa ilikwenda wapi, anadanya umma sasa hivi eti anataka kwenda Qatar, anahitaji kwenda Qatar? – Mch Peter Msigwa
 
Kwenye mistari mingine, mbunge huyu wa Iringa mjini 92.9 amesema hajahusika kuwatetea baadhi ya wamiliki wa vitalu vya wanyamapori kufuatia kuwa na hisa katika miradi hiyo.

No comments:

Post a Comment