Friday, March 29, 2013

BREAKING NEWS: JENGO LA GHOROFA 13 LAPOROMOKA JIJINI 

DAR ES SALAAM

.
.
.
.
.
.
.
.
Kwa maelezo ya shuhuda, inasemekana limeanguka saa moja asubuhi ambapo kwa muda huo kulikua na watoto wa kihindi wanacheza mpira, kulikua na vibarua ambao wanataka kumwaga zege kuendelea na ujenzi na ndio walikua wanabadilisha nguo kuanza kazi.

Ni posta mtaa wa Indira Gandhi pembeni ya msikiti mkubwa wa Itnasheri, lilikua ni gorofa la floor 12 ambapo mpaka sasa hakuna hesabu kamili ya vifo lakini shuhuda anasema kwa muda mfupi baada ya kuanguka alishuhudia maiti nne.

Sehemu ya chini zinaonekana bado nzima hazijadondoka ila kifusi cha kutoka juu ndio kimefunika lakini kuna watu ndani yake wako hai na inaripotiwa wanapata hewa vizuri na wamekua wakiwapigia ndugu zao na kuwaita waje kwenye eneo la tukio.

Endelea kuwa karibu na anaclet-ngoyi.blogspot.com taarifa zaidi zinazidi kufuatiliwa.
(kwahisani ya: millardayo.com)

No comments:

Post a Comment