Tuesday, January 29, 2013

RICKY ROSS ANUSURIKA KIFO BAADA YA KURUSHIWA RISASI

 Msanii Ricky Ross, leo asubuhi amenusurika kifo baada ya mtu mmoja aliekua na silaha kurusha risasi kadhaa kwenye gari aina ya Rolls Roys aliyokuwemo Ross na dem mmoja Ft. Lauderdale, Florida na kusababisha kugonga nyumba akijaribu kuongeza mwendo.
Ross hakupatwa na risasi hata moja wakati wa tukio hilo wala dem aliekuwa nae ndani ya gari hilo.
Ripoti zinadai risasi kibao zilirushwa kuelekea kwenye gari hilo mda wa saa kumi na moja asubuhi, na hakuna hata moja iliyoshoot kwenye Rolls.
polisi wanasema gari lingine lilisimama karibu na gari la Ross na mtu mmoja aliekuwa kwenye gari hilo kuanza kurusha risasi kwenye gari la Ross
 Mpaka sasa hakuna alietuhumiwa, kugundulika wala kushikiliwa juu ya tukio hilo

No comments:

Post a Comment