Tuesday, January 29, 2013

FRANK OCEAN ANATAKA KUFUNGUA MASHTAKA DHIDI YA CHRIS BROWN

frank_ocean_paparazzi 
Jana dunia iligubikwa na habari zilizozunguka kila kona ya mitandao ya jamii, zikielezea ugomvi  uliotekea siku ya jana, kati ya Chris Brown na msanii mwenzake wa r&b Frank Ocean, kwa kile kinachodaiwa ni kugombania parking ya gari katika studio za westlake.
stori iliyokuwepo ni kuwa, Frank alikasirika baada ya Chris Brown kupaki katika parking yake, na Chris Brown alizuiwa kutoka baada ya kumblock kwa nyuma, lakini ugomvi ulianza baada ya Chris brown kujaribu kushikana mkono na Frank Ocean.
chris_brown_angry
sasa the New York Post wameripot kuwa na habari isiyo nzuri baada ya Sheriff wa LA  kutoa repot ya kuwa, Frank anadhumuni la kufungua mashtaka kwa kumpiga ngumi na kuanzisha ugomvi nje ya studio za westlake, west Hollywood, jumapili asubuhi
Polisi wanataka kuongea na Brown ambae bado yupo brobation kwa kipigo alichompa Rihanna mwaka 2009.

No comments:

Post a Comment