Monday, April 1, 2013

CHALZ BABA AJITOLEA KUWASAPOTI BURE WALEMAVU WA SURVIVAL SISTERS, TAYARI AMESHAREKODI NAO SONGI MOJA NA VIDEO

 Wasanii wa Kundi la Survival Sisters, wakiwa jukwaani na Chalz Baba, katika moja ya shoo yan na Bendi ya Mashujaa Ijumaa iliyopita.
*************************************
MWIMBAJI na kiongozi wa bendi ya Mashujaa ya jijini Dar es Salaam, amejitolea kuwasaidia wasanii wa muziki wa dansi ambao ni walemavu wanaojulikana kwa jina la Survival Sisters, linaloundwa na wanadada watatu, lenye maskani yake Jijini Dar es Salaam.

Wasanii hao ni pamoja na Lucy Samson, Irene Mmbeka na Latifah Abdallah, ambao wote ni walemavu.

Akizungumza na mtandao huu wa www.sufianimafoto.com, Chalz Baba, alisema kuwa tayari mpaka sasa wamesharekodi wimbo mmoja unaokwenda kwa jina la Siambiwi 

Sisikii, uliorekodiwa katika Studio ya Metro, na video yake iliyokamilika tangu mwaka jana mwishoni ikirekodiwa katika studi za Kiumbe Video.

Wimbo huo pamoja na video tayari wameshausambaza katika vituo mbalimbali vya redio na Televisheni na inaendelea kufanya vizuri

Aidha wasanii hao kwa kushirikia na Chalz Baba, wapo mbioni kukamilisha albam yao itakayokuwa na jumla ya nyimbo Nane, ambayo itapewa jina baada ya kukamilika, huku ikitarajiwa kukamilika mnamo mwezi Oktoba mwaka huu. 

Chalz Baba, alisema kuwa mbali na yeye pia yupo katika mazungumzo na baadhi ya wasanii wengine, ili waweze pia kuwasaidia wasanii hao katika albam yao hiyo, ili kuweza kupata radha tofauti na kuweza kuuza na baadaye waweze kufikia malengo yao.

Katika kutambua umuhimu na kutambua mchango wa wasanii hao kaatika sanaa kutokana na akujituma kwao tofauti na walemavu wengine, Chalz Baba ameanzisha utaratibu wa kuzunguka nao katika baadhi ya shoo za bendi hiyo ya Mashujaa, ambapo kila siku ya Ijumaa na Jumapili kufaanya nao shoo ya pamoja katika Ukumbi wa Green Acres ulipo Victoria, ili waweze angalau kujipatia pesa kidogo za kujikimu.

Kutokana na hali halisi ya wasanii hao kutokuwa na uwezo wa kuingia Studio na kujilipia, wamekuwa wakidhaminiwa na baadhi ya studio kwa kupewa ofa ya kurekodi nyimbo kulingana na makubaliano na mwenye studio, na ndivyo hivyo wanavyotarajia kukamilisha albam yao hiyo kwa nia hiyo katika Studio mbalimbali zitakazojitolewa kuwasaidia.

Kundi hilo tayari lilifanikiwa kurekodi nyimbo tatu siku za nyuma na mbili kati ya hizo walizisambaza kwenye Vituo vya redio, lakini kwa bahati mbaya hazikuweza kufanya vizuri na kuwatambulisha kama walivyotarajia na sasa wanaamini kumpata msamaalia mwema kama Chalz Baba, sasa wanaweza kutambuka katika anga za muziki wa dansi kupitia jina lake, alisema mmoja wa wasanii haoLucy Samson.

Chalz Baba, aliwahasa wananii wengine wenye uwezo kujitokeza na kuwasaadia wasanii hao ambao wanauwezo wa kuimba na kushambulia jukwaa, ili waweze kutoka na kutambulika hata ikibidi Kitaifa na Kimataifa.

''Nawahaomba wanamuziki wenzangu na hata wasanii wa muziki wa Bongo Flava, wenye uwezo kujitokeza kuwasaidia wasanii hawa ili nao wajihisi ni miongoni mwa wanamuziki kama tulivyo sisi na waweze kutambulika zaidi katika kazi zao''. alisema Chalz Baba

No comments:

Post a Comment